
Video ya Utangulizi ya Kozi Mpya : Je, ujuzi wangu unawezaje kutumikia Kanisa? (Kiarabu chenye Manukuu ya Kiingereza)
Kila mmoja wenu atumie kipawa chochote alichopokea kuwatumikia wengine kama mawakili waaminifu wa neema ya Mungu katika namna mbalimbali. 1 Petro 4:10
aliye mkubwa miongoni mwenu atakuwa mtumishi wenu. Mathayo 23:11
Wengi wetu kwa kawaida hupendelea kuhudumiwa badala ya kuwahudumia wengine. Mara nyingi sana wale wanaohudumu katika ulimwengu huu hufanya hivyo kwa sababu wao ni maskini zaidi au duni kwa mamlaka au hadhi kuliko wale wanaohudumiwa.
Lakini Mwana mteule wa Mungu alikuja duniani akiwa mtumishi mnyenyekevu. Alitukomboa kwa dhabihu kuu kwake, hutuosha kutoka kwa dhambi zetu, na huturudisha katika ushirika na Baba yetu kama “warithi pamoja wa Ufalme wake”. Kisha, anatutayarisha na kututuma tukiwa watumishi wake ili kuwapenda wengine na kuwapatanisha na Baba, mpaka kila watu na kabila wawakilishwe katika Ufalme wake.
Katika kozi hii, tutachunguza maana ya kuwa mtumishi wa Kristo na kugundua baadhi ya njia tunaweza kumtumikia na kujenga ufalme wake tunapowafikia wengine.
Masomo
❶ Motisha Sahihi kwa Huduma Kuokolewa kwa neema kufanya matendo mema
❷ Wito wetu wa Juu kwa Huduma ya Unyenyekevu Kufuata mfano wa Kristo
❸ Lengo, Majaribu na Thawabu za Mtumishi Kukaza macho yetu juu ya kile ambacho ni cha milele
❹ Kuhudumia Familia ya Waumini Karama kwa ajili ya kulijenga Kanisa
❺ Kutumikia katika Ujirani Wetu Ili wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni
❻ Kutumikia kwaMiisho ya Dunia Kufanya kazi pamoja kufikia kila kabila
Kwa kupakua, kutumia, na/au kuwa na nyenzo za Kuendendelea Pamoja unakubali kutobadilisha nyenzo zetu na kuziwakilisha kama zako au kujaribu kuziuza kwa njia yoyote ile.
* Kumbuka: Sio programu zote za PDF zitaonyesha sehemu zinazoweza kuandikwa. Ikiwa una matatizo, tafadhali jaribu Adobe Acrobat Reader kutazama/kujaza faili ya PDF ya kozi.
