
Video ya Utangulizi ya Kozi Mpya : Je, ninashindaje uovu? (Kiarabu chenye Manukuu ya Kiingereza)
Hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Waefeso 6:10-11
Kila mwamini anajikuta katika mapambano ya kiroho dhidi ya nguvu za uovu (Waefeso 6:10-13). Ibilisi na mapepo yake, ingawa hayaonekani, wafanya hila na kutuchukulia hatua za uadui, wakijaribu kutuvuta mbali na Bwana, na hata kutuangamiza. Hata hivyo, Mungu hajatuacha bila ulinzi. Anatulinda na ametupa njia ya kuwapinga maadui hawa na kupata ushindi. Kwa hakika, Bwana tayari amewashinda adui zetu wa kiroho na ametupa ushindi wake. (Warumi 8:37-38). Mapambano haya dhidi ya majeshi ya kiroho ya uovu mara nyingi huitwa vita vya kiroho.
Uchawi, kwa upande mwingine, ni utafiti na ufuatiliaji wa nguvu hizi zilizofichwa, zisizo za kawaida kwa lengo la kuzitumia kwa manufaa ya kibinafsi. Kama utakavyoona, aina zote za uchawi ni milki ya shetani, na mwamini hapaswi kushiriki katika hizo. Inashangaza ni kiasi gani tamaduni zetu zinajumuisha aina mbalimbali za uchawi – iwe kwa siri au nje wazi – katika maisha ya kila siku. Kwa hiyo, utaona somo hili kuwa la vitendo na la lazima kwa matembezi yako na Bwana.
Masomo
- Bwana Yesu Kristo ana Mamlaka yote
- Nafasi Yetu katika Kristo
- Vifaa kwa ajili ya Vita vya Kiroho
- Kumpinga Ibilisi
- Kukataa Matendo ya Kichawi
Kwa kupakua, kutumia, na/au kuwa na nyenzo za Kuendendelea Pamoja unakubali kutobadilisha nyenzo zetu na kuziwakilisha kama zako au kujaribu kuziuza kwa njia yoyote ile.
* Kumbuka: Sio programu zote za PDF zitaonyesha sehemu zinazoweza kuandikwa. Ikiwa una matatizo, tafadhali jaribu Adobe Acrobat Reader kutazama/kujaza faili ya PDF ya kozi.
